Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Biashara zinazolipa zaidi Tanzania kwa mtaji mdogo

 Tuangalie biashara 21 za mtaji mdogo usiozidi Tshs. 100,000 unazoweza kufanya na zenye faida kubwa. Mtaji mkubwa unaohitajika unapoanzisha biashara ni muda na wala sio pesa kama utakavyojifunza hapa.



1. KUPIKA KWA 

Kama wewe ni mpishi mzuri au una mtu anayejua kupika, basi jitangaze kama unapokea oda za mapishi fulani

Tuchukulie unaweza kupika makande au wali nyama vizuri

Unachoweza kufanya ni kwenda maofisi ya karibu yako na kuwaambia kwamba wakutafute wanapohitaji hicho chakula wakati wa mchana na wewe utawaletea

Usisahau kuacha mawasiliano yako ili waweze kukutafuta

Wengi wao watapenda hiyo huduma kwasababu hawatohitaji kutoka tena kufata chakula

2. UREMBO (MAKEUP, KUSUKA & KUCHA

Urembo ni gharama. Wanadada wanataka kupendeza wanapokwenda safari zao kama ni kazini ama shughulini

Uzuri ni kwamba hii ni biashara ya kila siku unayoweza kufanya

Baada ya kufanya utafiti wangu, nimebaini kwamba kufanya makeup, kutengeneza kucha na ususi wa nywele zinalipa vizuri tu

Kuna watu wengi tu wanaendesha maisha yao kupitia biashara hizo. Kwanini wewe ushindwe? Na kama sio mtaalamu, hakuna tatizo

Chukua muda wako na kujifunza, ndani ya muda utaweza

3. KUUZA JUISI NA ICECREA

Kujifunza kutengeneza juisi au icecream haitakuchukuwa muda mrefu. Ili kufanikiwa katika biashara hii, cha muhimu ni kujitofautisha

Muhimu zaidi unapofanya biashara ya kutengeneza juisi au icecream, ni kuweka mazingira yako safi na salama kwa wateja wako

Uzuri wa biashara hii ni kuwa mtaji wake ni mdogo sana

Elfu kumi tu inatosha kuanzia na wapo waliofanya hivyo na wamekuza biashara zao kama vile Mak Juice au Zanana Juice Box

4. KILIMO CHA MBOGAMBOG

Kilimo ni sehemu kubwa ya maisha ya watanzania na wale wa nchi nyingi za Afrika

Kila siku zikienda, kilimo huzidi kuwa ni biashara ya matajiri kwasababu shamba lina gharama kubwa

Licha ya hivyo, bado kuna fursa ya kutengeneza kipato kupitia kilimo cha mbogamboga hata kama una mtaji mdogo

Anza na sehemu ndogo tu unayoweza kupata hata kama ni nyumbani

5. UFUGAJI WA NDEGE (KUKU, BATA, N.K

Hii ni biashara ambayo ina faida kubwa lakini pia ina changamoto zake kama vile kuku wako kufa

Vifo vya mifugo huwaumiza sana wafugaji na mara nyingi husababishwa na mifugo hiyo kula uchafu

Hivyo, unapoingia kwenye ufugaji jitahidi uwe na mazingira safi na salama kwa mifugo yako

Usafi wa mara kwa mara hasa hasa kwenye malisho yao utahitajika

Kwa vile mtaji ni mdogo, unaweza kuanza na kuku wa kienyeji, bata au hata njiwa. Japo kuwa wanachukuwa muda ila kuwa mvumilivu, faida utaiona

6. KUPIGA PICH

Tangu kuja kwa mitandao ya jamii kama vile Instagram, watumiaji wa mitandao hiyo hutaka picha nzuri

Hapo ndipo unapojitokeza wewe na kuwapa huduma yako ya kupiga picha

Upigaji wa picha ni fani kama fani yengine, ili ujitofautishe pendelea kujifunza kwa wanaojua au tumia YouTube kujifunza

Vifaa vya upigaji picha vina gharama ila sio lazima viwe vyako, muhimu ni kuwa na ujuzi. Vifaa unaweza kumuazima rafiki yako au kukodi

7. KUTENGENEZA TOVUTI (WEBSITES

Tuko katika ulimwengu wa habari na teknolojia, hivyo kampuni ama biashara ambayo hawako mtandaoni wanakosa wateja

Ichangamkie fursa hiyo kwa kujifunza kutengeneza websites kupitia YouTube

Kisha, tafuta biashara/ makampuni ambayo hawana tovuti na uwaelezee umuhimu wa kuwa na tovuti

Mwisho, waambie kuwa wewe unatoa huduma hiyo

Kwa kuanza, wateja wako wa mwanzo unaweza kuwafanyia kwa bei ya punguzo halafu mbeleni ukapandisha. Njia hii itakusaidia kupata mabalozi watakao kupatia wateja wengine

8. KUPANGA SHEREHE/MATUKIO (EVENT PLANNING

Kuanzia maharusi, kitchen party, sandoff na sherehe nyenginezo nisizozifahamu. Zote hizi ni fursa ambapo unaenda kusaidia watu kuandaa sherehe zao mwanzo mpaka mwisho

Wewe ndio unaumiza kichwa kutafuta watu na huduma mbalimbali kama vile wapambaji, ma dj, au kuwatafutia gari ya kukodi, kuwapikishia chakula na megine mengi

Unachohitaji kuweza kufanya biashara hii ni uwe unawajua watu husika wanaotakiwa kwenye sherehe hizo

Mfano, ujue wapambaji wa ukumbi, wapishi wa maharusi, ma dj ili uweze kuwapa kazi hizo. Utalipwa kwa kufanya kazi hiyo

9. KUTEMBEZA WATALI

Hii nayo ni biashara nyengine ambayo haihitaji pesa kabisa

Unachohitaji ni kufahamu historia ya nchi yako hasa hasa ile ya maeneo ambayo watalii wanapenda kwenda

Mfano, Zanzibar mtembeza watalii anaweza kulipwa kuanzia elfu ishirini kwa safari moja. Kwa siku ukipata safari tano tu unaondoka na zaidi ya laki moja

10. USHONAJI NGU

Kama wewe ni mpenzi wa mitindo, unaweza tengeneza kipato kizuri kwa kuwashonea watu nguo

Itakuchukuwa muda kujifunza kushona ila ni kazi moja nzuri. Unapata kuwa mbunifu katika kutengeneza mishono mbali mbali na mwisho wake kulipwa

Kama huna cherehani nyumbani, unaweza kwenda kukodi na kufanyia kazi zako hadi utakapo nunua yako

11. KUFUNDISH

Unaweza kufundisha chochote kila unachokijua ikiwa kuna watu wanataka kujifunza

Jitathmini kwa kujiuliza, je ni kitu gani nakijua ambacho watu wanataka kujifunza? Hiyo ni rasilimali tosha

Watafute hao watu na uwape huduma zako. Taaluma sio lazima iwe kufundisha hesabati na kemia tu, kama unajua kupika vizuri, kushona au chochote kile basi wafundishe watu

12. KUTENGENEZA SIMU/KOMPYUT

Watumiaji wa vifaa kama vile simu na kompyuta huzidi kila siku

Vifaa hivi vinapopata tatizo kama vile kuingia loki sio kila mtu anaweza kutengeneza mwenyewe

Hiyo hukupa wewe fursa ya kuwatatulia matatizo yao kwa kiasi cha pesa kadhaa. Unaweza kujifunza jinsi ya kutengeneza matatizo sugu ya simu kwenye mtandao

13. UNYOZI WA NYWEL

Hii pia ni biashara isiyokuwa na msimu kwavile nywele huota kila siku

Jifunze kunyoa watu nywele halafu anza na wale wakaribu yako kama vile marafiki na ndugu

Utakapofanya kazi nzuri hao watakuwa wateja wako wakujirudia na pia kukutangazia huduma zako kwa watu wengine

Unachohitaji ni kununua mashine ya kunyolea ambayo unaweza kupata kwa chini ya elfu hamsini

14. KUNUNUA NA KUUZA BIDHA

Sifa ya kubwa ya mjasiriamali ni kuona thamani ya vitu kabla wengine hawajaviona

Hivyo, tafuta bidhaa ambazo zinauzwa kwa bei ya chini, zinunue na utafute soko ambalo hizo bidhaa zinauzwa kwa bei ya juu uende ukaziuze huko

Mfano, unaweza kutoa bidhaa Dar es Salaam ukaja kuuza Zanzibar na kinyume chake pia inawezekana

15. KUUZA VOCHA ZA SIM

Vocha! Tunanunua karibia kila siku

Faida yake sio kubwa kihivyo ila ukizingatia kazi ni ndogo ya kufanya kwasababu vocha zinajiuza wenyewe

Vocha sio kitu cha kutumia nguvu kuuza muhimu watu wajue tu kama unauza vocha

Unaweza kuona vocha zinauzwa kila sehemu kwamba utakosa wateja … lakini sio kweli, kuna sehemu nyingi tu ambazo hakuna muuza vocha karibu

Anza kuwauzia watu unaoishi nao, majirani au hata wanafunzi wa chuo

16. UFUGAJI WA SAMAK

Ufugaji wa samaki uko wa aina mbili, kuna samaki wa kula na wale wa mapambo. Hapa nitaongelea samaki wa mapambo kwa vile wana gharama ndogo na pia faida kubwa

Unaweza anza na samaki wawili au wanne na kuwatunza. Wakizaliana na kuwa wengi, uza baadhi yao

17. KUKUZA MITI YA MAU

Maua hupendezesha nyumba na wengi huamua kupanda nyumbani kwao

Fuatilia jinsi gani maua tofauti yanavyopandwa na kisha yapande

Kwa wastani, mti mmoja wa maua huuzwa kuanzia elfu mbili. Mtaji mkubwa hapa ni muda wa kupanda na kuishughulikia hiyo miti

18. KUFANYA USAFI MAJUMBANI NA MAOFISIN

Watu wengi wamebanwa na kazi, na muda wasiokuwa kazini wana mambo mengi ya kufanya

Unaweza kuwafanyia usafi na wakakulipa. Ni vizuri ukanunua vifaa vyako ambavyo sio ghali ila sehemu nyingi watakuruhusu kutumia vifaa vyao vya usafi

Biashara ikiwa kubwa, unaweza amua kutafuta vifaa tofauti tofauti vya kufanyia kazi kitaalamu zaidi

19. KOCHA WA MAZOEZ

Nathubutu kusema kuwa hakuna kitu chenye thamani kwenye maisha kama afya nzuri

Watu wengi wanashtuka sikuhizi juu ya umuhimu wa kula vizuri na kufanya mazoezi. Hivyo, baada ya kupata elimu nzuri ya mazoezi, anza kawafundisha watu. Utalipwa kwa ujuzi na muda wako

20. KUPAMBA MAHARUS

Harusi ni biashara kubwa

Hivi, nani hapendi kupendeza siku ya harusi yake? Hamna. Na ili kupendeza harusini, wanandoa inabidi wapambwe

Tafuta mtu anayepamba maharusi na muombe kumfanyia kazi (ikiwezekana bila hata malipo). Baada ya muda utajifunza vitu vingi vitakavyo kusaidia kuwa mtaalamu wa kupamba maharusi

21. KUWAUZIA WATU BIDHAA ZA

Kwa akili ya kawaida, ni rahisi mtu kukulipa unapomtengenezea pesa

Jifuze kuuza kisha tafuta watu wenye biashara na uwaambie kuwa unaweza kuwaletea wateja kwa malipo mutakayokubaliana

Hii ni biashara nzuri kwasababu unatengeneza kipato kwa kutumia fedha ya mtu mwengine. Unachohitaji ni ujuzi wa kuuza vitu..O...I..I...I...A..I.....U...A....E...A...A...O...I....).....)....A.....)....A....M.....).....ODAasababu unatengeneza kipato kwa kutumia fedha ya mtu mwengine. Unachohitaji ni ujuzi wa kuuza vitu.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Njia mbalimbali za kuandika tangazo la biashara

Ikiwa ni mfanyabiashara jifunze jinsi ya kuwashawishi wateja na kupata matokeo.unatakiwa kutangaza kupata matokeo makubwa watu wavutiwe na bidhaa zako na kuwafanya wateja kuwa na hamu kubwa ya kununua bidhaa zako Jifunze njia mbalimbali za kuandika tangazo la kuuza bidhaa/huduma mtandaoni 1.Andika kama vile jinsi unavyoongea Kampuni yako au bidhaa yako ni kama mtu na inasifa yakuwa na sauti. Na tumia hiyo sauti kuifuatisha Andika tangazo kama vile unavyoweza kuzungumza,maneno utayoandika kati ya kampuni yako na mnunuzi wako Sauti yako na hasa maneno utayochagua kutumia yatakuwa tofauti sana 2.Andika sifa na faida kabla haujaanza Watu hawawezi kununua bidhaa yako au huduma yako ikiwa hawafahamu watanufaika na nini kwenye bidhaa yako. Mfano unauza  printer waelimishe watu huduma yako itawasaidiaje, je inaokoa mda na kazi? Ubora wa hiyo bidhaa yako? Unamwambia nini mteja ategemee kwenye hiyo bidhaa? Andika sifa na faida kwa mteja kile ambacho atanufaika kuhusu bidhaa au hu...

Mambo yakuzingatia unapotaka kuuza mafuta ya ngozi ya mafuta kwa wateja wa jumla

Makampuni mengi lengo lao kubwa ni kuuza bidhaa zao za mafuta ya ngozi jumla kwa wateja wanaoenda kuuza rejareja. Hatua hii inaweza kuwa changamoto kwa wazalishaji wa bidhaa na wauzaji ili uweze kufanya mauzo vizuri na ufanikiwe kuwapata wanunuzi wa bidhaa yako inatakiwa ufanye maandalizi na ujue nini unategemea Kufanikiwa kufikisha na kuuza bidhaa za mafuta ya ngozi kwa wanunuaji fuata hatua chache na kuwa na ujuzi .kiujumla kampuni inaweza kuwa kubwa ,ikawepo mtandaoni lakini watu wangapi nao wanafanya hivyo Weka mipango vizuri kuhusu wateja,ushindani,na brand izidi kukuwa. Pia kuwa makini wakati wa kuuza na kufanya mapatano ya bei. Mwisho biashara yako itakuwa na itapanuka Mambo yakuzingatia unapotaka kuuza mafuta ya ngozi kwa bei ya jumla 1. Wanunuaji huwa wanaangalia bidhaa yenye ubunifu Inatakiwa uuze bidhaa ambayo mtu atataka kununua . Pengine inaweza ikawa na ubunifu katika kifungashio,vitu vilivyotumika kutengenezea,technolojia,inavyotumika etc  inatakiwa uongeze t...

Mambo ya kuzingatia unapotaka kuuza gari used mtandaoni

Kuna watu wengi wanauza magari kupitia mtandao wanatangaza biashara kupitia mitandao mikubwa hapa Tanzania kama guliostore.com , Kupatana na ZoomTanzania, na   ni njia ya kupata wateja wengi zaidi baada ya kuchagua tovuti ya kutaka kutangaza biashara  osha gari lako kisha chukua picha nyingi zakupost mtandaoni Kama mteja atakutafuta utamwambia maongezi ya bei utofauti wa bei na wauzaji wenzio itategemea na gari yako ina hali gani Hapa leo tumekuletea mambo yakuzingatia unapotaka kuuza gari used mtandaoni 1.Hakikisha una kadi ya gari Mara unavyoweka gari lako mtandaoni wateja wengi wataanza kukutafuta. Kabla haujaanza kutangaza mtandaoni hakikisha gari yako unavielelezo vyote kuwa wewe ndio mmiliki pia lipia mapato yako yote ikiwa kama unadaiwa 2.Elewa kipi unakijua kuhusu gari yako Mara mtu anapoanza kukutafuta huwa anakuja na maswali mengi utafanya  vizuri kuwajibu Ikiwa hauna ujuzi wowote ni muda sasa wakuanza kufuatilia gari yako ina engine ya aina g...