Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Hizi ndio biashara zenye faida zaidi Tanzania

 1. Migahawa na Fast food





Angalau kila binadamu anatakiwa kula chakula ili aweze kuishi. Maeneneo makubwa ya miji kama Nairobi, Kampala na Dar es salaam yanakua kwa kasi na hivyo idadi ya watu kuwa kubwa zaidi. Wafanyabiashara wengi wanaofanya biashara hii kiufasaha wanaweza kukua zaidi na kuwa na biashara kubwa sana.




2. Tiba Asili.

Kama ilivyo kwa nchi nyingi Afrika tiba asili zimekuwa zikiaminika kuwa bora zaidi. Hata nchi za wenzetu walioendelea kama China hupenda dawa za asili kwani hazina kemikali. Siyo kila mtu anaweza kufanya biashara hizi. Huhitaji uzoefu na lazima upate idhini ya serikali kama tiba ni salama.


3. Saluni na Urembo.

Siku hizi masuala kama Pedicure, Manicure na masaji yamekuwa mambo yanayotiliwa maanani na jamii za wa Afrika mashariki. Hair dressing na kunyoa ni kama mambo ya lazima kwa mtu yeyote mwenye kuhitaji kuwa mtanashati. Biashara hii inaendelea kuwanufaisha wengi kama ukitoa huduma nzuri na za kipekee.





4. Famasia na Madawa.

Ili kufanya biashara hii utahitaji elimu na uzoefu lakini faida utaipata. Magonjwa hayaishi. Hivyo watu wanaofanya biashara hii ya kuuza madawa na vifaa vya famasia wamekuwa wakipata mapato mazuri na faida kwa ni biashara yenye uhakika wa kuuzika.


5. Vifaa vya ujenzi.

Watu wanajenga kila siku. Vifaa vya ujenzi hununuliwa na kuisha kabisa madukani. Viwanda haviishii kutengeza bidhaa. Nani hapendi ujenzi?



6. Vito vya thamani.

Urembo ni jadi ya waafrika waliojaliwa ubinufu wa mawazi na kuwa wenye muonekano mzuri kwa watu. Zaidi biashara ya vito vya thamani huwavutia pia watu wa mataifa yote duniani. Biashara hii inashika nafasi ya kati (5/10) katika biashara zetu kumi zenye malipo bomba zaidi Afrika mashariki.


7. Vifaa vya uani.

Vifaa kama Toilet paper, diaper za watoto, dawa za choonin na sabuni zimeshika kasi katika soko ukanda huu wa Afrika Mashariki. Vitu kama tissue hutumika mahotelini na katika hafa mbalimbaili kama unahitaji kupiga bao, chukua fursa hii.


8 .Pombe na Vilevi. 


Makampuni kama TBL yamefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika kufanya biashara hii. Vilevi vingine kutoka nje ya nchi vimepata umaarufu sana Afrika Mashariki. Sababu kubwa ni kwamba watu wanapenda kuburudika ndio maana ukianzisha biashara ya kuuza vinywaji hivi utafanikiwa.


9. Vifaa vya Elektroniki.

Hii ni moja kati ya biashara kubwa mbili ukanda huu. Tanzania pekee inaongoza kwa watu wengi kumiliki simu za mkononi. Biashara ya vifaa vya elektroniki Afrika Mashariki inalipa kwa kiasi kikubwa sana. Fikiri vifaa kama friji, computer. Mjasiriamali mwenye malengo haswa ataipenda zaidi biashara hii.


10. Vipodozi.

Bila shaka bingwa ndiye huyu. Hii ni biashara yenye mauzo makubwa zaidi Afrika Mashariki. Wanawake wengi hupenda kutumia vipodozi. Jumla ya idadi ya wanawake ni kubwa sana ukilinganisha na idadi ya wanaume Afrika Mashariki. Wanaume pia hununua vipodozi. Kama hauna uhakika ni biashara gani uanzishe, hili ndilo kimbilio lako.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Njia mbalimbali za kuandika tangazo la biashara

Ikiwa ni mfanyabiashara jifunze jinsi ya kuwashawishi wateja na kupata matokeo.unatakiwa kutangaza kupata matokeo makubwa watu wavutiwe na bidhaa zako na kuwafanya wateja kuwa na hamu kubwa ya kununua bidhaa zako Jifunze njia mbalimbali za kuandika tangazo la kuuza bidhaa/huduma mtandaoni 1.Andika kama vile jinsi unavyoongea Kampuni yako au bidhaa yako ni kama mtu na inasifa yakuwa na sauti. Na tumia hiyo sauti kuifuatisha Andika tangazo kama vile unavyoweza kuzungumza,maneno utayoandika kati ya kampuni yako na mnunuzi wako Sauti yako na hasa maneno utayochagua kutumia yatakuwa tofauti sana 2.Andika sifa na faida kabla haujaanza Watu hawawezi kununua bidhaa yako au huduma yako ikiwa hawafahamu watanufaika na nini kwenye bidhaa yako. Mfano unauza  printer waelimishe watu huduma yako itawasaidiaje, je inaokoa mda na kazi? Ubora wa hiyo bidhaa yako? Unamwambia nini mteja ategemee kwenye hiyo bidhaa? Andika sifa na faida kwa mteja kile ambacho atanufaika kuhusu bidhaa au hu...

Mambo yakuzingatia unapotaka kuuza mafuta ya ngozi ya mafuta kwa wateja wa jumla

Makampuni mengi lengo lao kubwa ni kuuza bidhaa zao za mafuta ya ngozi jumla kwa wateja wanaoenda kuuza rejareja. Hatua hii inaweza kuwa changamoto kwa wazalishaji wa bidhaa na wauzaji ili uweze kufanya mauzo vizuri na ufanikiwe kuwapata wanunuzi wa bidhaa yako inatakiwa ufanye maandalizi na ujue nini unategemea Kufanikiwa kufikisha na kuuza bidhaa za mafuta ya ngozi kwa wanunuaji fuata hatua chache na kuwa na ujuzi .kiujumla kampuni inaweza kuwa kubwa ,ikawepo mtandaoni lakini watu wangapi nao wanafanya hivyo Weka mipango vizuri kuhusu wateja,ushindani,na brand izidi kukuwa. Pia kuwa makini wakati wa kuuza na kufanya mapatano ya bei. Mwisho biashara yako itakuwa na itapanuka Mambo yakuzingatia unapotaka kuuza mafuta ya ngozi kwa bei ya jumla 1. Wanunuaji huwa wanaangalia bidhaa yenye ubunifu Inatakiwa uuze bidhaa ambayo mtu atataka kununua . Pengine inaweza ikawa na ubunifu katika kifungashio,vitu vilivyotumika kutengenezea,technolojia,inavyotumika etc  inatakiwa uongeze t...

Mambo ya kuzingatia unapotaka kuuza gari used mtandaoni

Kuna watu wengi wanauza magari kupitia mtandao wanatangaza biashara kupitia mitandao mikubwa hapa Tanzania kama guliostore.com , Kupatana na ZoomTanzania, na   ni njia ya kupata wateja wengi zaidi baada ya kuchagua tovuti ya kutaka kutangaza biashara  osha gari lako kisha chukua picha nyingi zakupost mtandaoni Kama mteja atakutafuta utamwambia maongezi ya bei utofauti wa bei na wauzaji wenzio itategemea na gari yako ina hali gani Hapa leo tumekuletea mambo yakuzingatia unapotaka kuuza gari used mtandaoni 1.Hakikisha una kadi ya gari Mara unavyoweka gari lako mtandaoni wateja wengi wataanza kukutafuta. Kabla haujaanza kutangaza mtandaoni hakikisha gari yako unavielelezo vyote kuwa wewe ndio mmiliki pia lipia mapato yako yote ikiwa kama unadaiwa 2.Elewa kipi unakijua kuhusu gari yako Mara mtu anapoanza kukutafuta huwa anakuja na maswali mengi utafanya  vizuri kuwajibu Ikiwa hauna ujuzi wowote ni muda sasa wakuanza kufuatilia gari yako ina engine ya aina g...