Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Ukifanya biashara hizi utapata faida zaidi ya 50000 kwa siku

 Ukifanya biashara hizi utapata faida zaidi ya 50000 kwa siku


1.Biashara ya kuuza samaki

Biashara hii inafaa zaidi kuifanya kwenye majiji makubwa


Tafuta meza maeneo yenye junction au karibu na kituo cha daladala, (eneo lililochangamka kama Mbagala, Buguruni etc)

Nenda ferry kanunue Pweza, ngisi na kamba. Wapike kwa ustadi wa hali ya juu, tumia akili zote kuja na kitu kinachovutia. Uza Supu ya pweza etc, nakuhakilishia, utapata faida zaidi ya 25% ya mtaji wako!


Ukishapata uzoefu, fanya branding kabisa, tafuta kibanda kidogo, kitengeneze vizuri, weka bango andika supu ya pweza! Utapata wateja wa kutosha sana!

 

2.Biashara ya kuuza mkaa


biashara ya mkaa mkuu hautojutia, kama upo karbu na handeni unaweza fanya proces za kuchoma mkaa angalau uanze na gunia 150 ambapo gharama za kuchoma sio chini ya laki5 na gharama za kusafirisha mpaka dar kila gunia ni 6k

kibali cha tfs laki mbil kwa mwaka

gharama za kibanda hapa dsm unaeza pata kuanzia elf 30 mpk 40 kwa mwez kodi ya pango

kila gunia hapa dsm lnauzwa elfu 25 mpka 30 kama ukibahatika kuuza gunia 3 au 4 kwa siku hyo utakuwa na faida ya uhakika

25000*4=100k

faida katika kila gunia ni sh 10k mpk 15k


3. Biashara ya kuuza mazao ya chakula


Biashara ya nafaka inalipa. unaweza jikita na mazao kama maharagwe, kunde, njegere, mbaazi nk. mtaji unategemea na uhitaji, anza hata kidogo kwa gunia kama 3 kwa kila zao ila fanya utafiti wa soko ili utakapotaka kujitanua isikupe tabu.


Pia unaweza kuyaongezea thamani hayo mazao kama vile kugred na kupark kabisa. Hapo utakuwa umeongeza thamani na utauza kwa bei ya juu, na unaweza tafuta hata supermaket tano tu za kuwa sambazia


4. Biashara ya kuuza viatu vya mtumba


Hii ni biashara pia yenye faida kubwa inayoweza kukutajirisha na kukutoa kabisa kwenye hali ngumu. Biashara hii inahitaji mtaji mdogo tu kuanzia Tsh 50000-1000000 


Masoko ya viatu vya mtumba unakoweza kupata kwa bei nzuri ni dar maeneo ya karume kiatu utakachonunua kwa Tsh 5000 utauza mpaka Tsh 20000-30000 hapa utaona ni namna gani biashara hii inafaida


5.Biashara ya kuuza juisi ya miwa


Kuanza biashara hii mambo yafuatayo ni ya msingi kuzingatia:


1) Mashine ya kukamua miwa – Tsh 300,000-400,000

2) Glasi nzuri za ujazo tofauti – Tsh 20,000

3) Chujio – Tsh 5,000

4) Beseni – Tsh 8,000

6) Ndoo 2 – Tsh 5,000

7) Jaba kubwa la uchafu – Tsh 12,000

8) Mtaji wa kununua miwa –Tsh 50,000

9) Tolori la kusafirisha – Tsh 60,000

10) Vifaa vingine – Tsh 40,000

Jumla ya mtaji wa kuanzia Tsh 640,000/=


Muwa mmoja unaweza ukatengeneza lita 4 za juisi na muwa mmoja unaweza ukaununua kwa Tsh.300/= kwa bei ya jumla. Lita moja ya juisi utauza 1,000/= hivyo kwa muwa mmoja unatengeneza Ths 4,000/=.


6. Biashara ya kuuza chips

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Njia mbalimbali za kuandika tangazo la biashara

Ikiwa ni mfanyabiashara jifunze jinsi ya kuwashawishi wateja na kupata matokeo.unatakiwa kutangaza kupata matokeo makubwa watu wavutiwe na bidhaa zako na kuwafanya wateja kuwa na hamu kubwa ya kununua bidhaa zako Jifunze njia mbalimbali za kuandika tangazo la kuuza bidhaa/huduma mtandaoni 1.Andika kama vile jinsi unavyoongea Kampuni yako au bidhaa yako ni kama mtu na inasifa yakuwa na sauti. Na tumia hiyo sauti kuifuatisha Andika tangazo kama vile unavyoweza kuzungumza,maneno utayoandika kati ya kampuni yako na mnunuzi wako Sauti yako na hasa maneno utayochagua kutumia yatakuwa tofauti sana 2.Andika sifa na faida kabla haujaanza Watu hawawezi kununua bidhaa yako au huduma yako ikiwa hawafahamu watanufaika na nini kwenye bidhaa yako. Mfano unauza  printer waelimishe watu huduma yako itawasaidiaje, je inaokoa mda na kazi? Ubora wa hiyo bidhaa yako? Unamwambia nini mteja ategemee kwenye hiyo bidhaa? Andika sifa na faida kwa mteja kile ambacho atanufaika kuhusu bidhaa au hu...

Mambo yakuzingatia unapotaka kuuza mafuta ya ngozi ya mafuta kwa wateja wa jumla

Makampuni mengi lengo lao kubwa ni kuuza bidhaa zao za mafuta ya ngozi jumla kwa wateja wanaoenda kuuza rejareja. Hatua hii inaweza kuwa changamoto kwa wazalishaji wa bidhaa na wauzaji ili uweze kufanya mauzo vizuri na ufanikiwe kuwapata wanunuzi wa bidhaa yako inatakiwa ufanye maandalizi na ujue nini unategemea Kufanikiwa kufikisha na kuuza bidhaa za mafuta ya ngozi kwa wanunuaji fuata hatua chache na kuwa na ujuzi .kiujumla kampuni inaweza kuwa kubwa ,ikawepo mtandaoni lakini watu wangapi nao wanafanya hivyo Weka mipango vizuri kuhusu wateja,ushindani,na brand izidi kukuwa. Pia kuwa makini wakati wa kuuza na kufanya mapatano ya bei. Mwisho biashara yako itakuwa na itapanuka Mambo yakuzingatia unapotaka kuuza mafuta ya ngozi kwa bei ya jumla 1. Wanunuaji huwa wanaangalia bidhaa yenye ubunifu Inatakiwa uuze bidhaa ambayo mtu atataka kununua . Pengine inaweza ikawa na ubunifu katika kifungashio,vitu vilivyotumika kutengenezea,technolojia,inavyotumika etc  inatakiwa uongeze t...

Mambo ya kuzingatia unapotaka kuuza gari used mtandaoni

Kuna watu wengi wanauza magari kupitia mtandao wanatangaza biashara kupitia mitandao mikubwa hapa Tanzania kama guliostore.com , Kupatana na ZoomTanzania, na   ni njia ya kupata wateja wengi zaidi baada ya kuchagua tovuti ya kutaka kutangaza biashara  osha gari lako kisha chukua picha nyingi zakupost mtandaoni Kama mteja atakutafuta utamwambia maongezi ya bei utofauti wa bei na wauzaji wenzio itategemea na gari yako ina hali gani Hapa leo tumekuletea mambo yakuzingatia unapotaka kuuza gari used mtandaoni 1.Hakikisha una kadi ya gari Mara unavyoweka gari lako mtandaoni wateja wengi wataanza kukutafuta. Kabla haujaanza kutangaza mtandaoni hakikisha gari yako unavielelezo vyote kuwa wewe ndio mmiliki pia lipia mapato yako yote ikiwa kama unadaiwa 2.Elewa kipi unakijua kuhusu gari yako Mara mtu anapoanza kukutafuta huwa anakuja na maswali mengi utafanya  vizuri kuwajibu Ikiwa hauna ujuzi wowote ni muda sasa wakuanza kufuatilia gari yako ina engine ya aina g...